Saturday, 14 May 2016

HARMONIZE FT RAY - PENZI

                    VERSE 1: Ray
Nawaza kwanini sikumjuaga zamani
                ( Ooh mama )
Pendo lake zito mpaka lavunja mizani
                ( Ooh mama )
yeye na Mimi kacho nisharuka nyie
                 ( ooh mama )
Wasiojua mapenzi pole jamani
Eti alikuwa bachelor aibu gani

                   Harmonize:
Aliyeumba dunia,akayaumba na mapenzi
Wala hakukosea,ila mwenzenu mi cwezi
Nilishapenda,ila nikatendwa
Moyo ulidunda,masikini roho
Mbona nilikonda,licha ya kuhonga
kuweka vibanda,nishaomba poo
Mwenzangu bado ujajua,baki unicheke
Kwako yamechanua Ngoja yanyauke

                   Ray
Andazi si kitumbua,acha mapepe
Ukipendwa tanua,kwanini nsideke

                    CHORUS :
                        Ray
Jama nimependa mimi,nimependa Mimi
Nimependa Mimi,nataka nimuweke ndani

                       Harmonize
Mwenzako nimetendwa mie,nimetendwa mie
Nimetendwa mie,mapenzi siyatamani
    
                         Ray
Jama nimependa Mimi,nimependa Mimi
Nimependa mimi,nataka nimuweke ndani

                         Harmonize
mwenzako nimetendwa mie,nimetendwa mie
Nimetendwa mie,mapenzi siyatamani

                      VERSE 2: Ray
Ana mapenzi ya bara kachanganya na pwani
Vipi nitajinasua..!? rangi kama chotara
shepu sio mjapani, marashi huzibi pua
Aaah Ameumbika sina budi nisifie
akipika natamani nilipie
sehemu ya upanga uliweka kiwembe
ndo maana mwasi akaona ajichenge

                      Harmonize
Kwa wenzako sikia,sikia Mwana
Ila kwako utalia utalia sana
Mi nilikuwaga fundi,fundi zaidi yako
Power ka milundi,nikiganda kama sumako
nakutia pesa madegeje,asiniache
Nikamchanganya akolee,asiwake
Penzi upepo Wa bahari,Mara kusi shwari
Yakichange hatari,na usiombe

                       CHORUS : Ray
Jama nimependa Mimi,nimependa Mimi
nimependa Mimi,nataka nimuweke ndani

                       Harmonize
mwenzako nimetendwa mie,nimetendwa mie
Nimetendwa mie,mapenzi siyatamani

                       Ray
Jama nimependa mimi,nimependa Mimi
Nimependa Mimi,nataka nimuweke ndani

                     Harmonize
mwenzako nimetendwa mie,nimetendwa mie
nimetendwa mie,mapenzi siyatamani

                       ( OUTRO ) Ray
nimependa Mimi,nimependa mimi
Nimependa Mimi,nimependa Mimi

                       Harmonize
Nimetendwa mie,nimetendwa mie
Nimetendwa mie,nimetendwa mie

          
                       

No comments:

Post a Comment